Sunday, April 23, 2017

WAUGUZI HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI WASHEHEREHEKEA GET TOGETHER PARTY 2017

Mkurugenzi wa Uuguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Agnes Mtawa (wa tano kushoto) katika picha ya pamoja na baadhi ya wauguzi wa hospitali hiyo Dae es Salaam Jana April 22, 2017. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA) Mmiliki wa ujijirahaa blog
 
Mkurugenzi wa Uuguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Agnes Mtawa (wa nne kulia)  akigonganisha Glas zenye kinyaji cha shampeni na Wakuu wa vitengo mbalimbali wa  Hospitali hiyo

 
Baadhi ya Wakuu wa Idara na wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili wakiwa katika Gari kuelekea katika kusheherekea sherehe yao iliyofanyika Navy Beach Kigamboni Dar es Salaam jana
Baadhi ya wanakamati wakiwa katika picha ya pamoja wakiongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Segla Mgaya (wa tano kushoto) ambaye ni Afisa Muuguzi wa hospitali hiyo  
Mkurugenzi wa Uuguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH, Agnes Mtawa  akizungumza na wauguzi hao wakati wa kusheherehekea Get Together Party 2017 iliyofanyika Dar es Salaam jana April 22, katika Ukumbi wa Navy Beach Kigamboni  ambapo alipata nafasi ya kuanza kutowa  salamu kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo,  Profesa Lawrence Museru kwakutofika,
 
Mtawa alisema, pokeeni salamkutoka kwa mpendwa wetu Mkurugenzi,  anawasalimia sana na kuwatakia heri katika sherehe hii na amesema Mungu akitupa uzima mwakani anaomba taarifa apate mapema iliaweze kuserebuka nasi na kwakumalizia salamu hizo alisema  pia naomba mpoke salam zake
Mkurugenzi wa Uuguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili, Agnes Mtawa (kushoto) akipokea Ua kutoka kwa mtunza hazina wa Kamati hiyo, Matilda Mrina ambaye ni Afisa Mkuu Msaidizi Daraja la Kwanza 
Meneja wa Jengo la Mwaisela, Unyanjite Hema akicheza mchezo wa karata na Muuguzi, Debora Bukuku wakati wa Sherehe hiyo
Mkurugenzi wa Uuguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili, Agnes Mtawa akizindua mchezo wa mazoezi kwa kuruka kamba mbele ya Wauguzi (pichani hawapo) wakati wa kusheherehekea, Get Together Party 2017 iliyofanyika Dar es Salaam jana April 22, 2017 katika Ukumbi wa Navy Beach Kigamboni , ambapo kulikuwa na michezo mbalimbali ya kuchangamsha mwili ikiwemo, kuruka kamba, kucheza karata, kuogele, kucheza mpira na Burudani ya nyimbo mbalimbali kutoka kwa kikundi cha wasanii cha wauguzi kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, michezo hiyo iliyoratibiwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Segla Mgaya
Mkurugenzi wa Uuguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili, Agnes Mtawa (wa pili kushoto) akisindikizwa na wauguzi hao na wapilikulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Segla Mgaya


Muuguzi wa Hospitali hiyo, Vaileth Minja akifungua Sherehe hiyo kwa Salaa
 
Wauguzi wakicheza


Mkurugenzi Agnes Mtwa akicheza pamoja na wauguzi hao
Mkurugenzi wa Uuguzi, Agnes Mtawa (mwenye mkanda mweusi tumboni) akionyesha umahiri wake kwa kucheza  kwaito na  wauguzi hao

Mwenyekiti wa Kamati hiho, Segla Mgaya  akiwa katika picha ya pamoja na Wauguzi hao
Meneja wa Tawi la Benk NMB Muhimbili, (jina halikupatikana mara moja) akizungumza na wauguzi hao akisisitiza, anaomba kushirikiana na Wauguzi hao, hayo aliyasema wakati wa Sherehe ya Get Together Party 2017, iliyofanyika Dar es Salaam jana katika Ukumbi wa Navy Beach Kigamboni, alianza kwa kusema, 
 
Sisi wana wa NMB tunaamini kwa wafanyakazi wanapokutana kwa pamoja wanaongeza ufanisi wa kazi kwa sababu wanakutana pamoja na wanapokuwa Muhimbili kila mmoja anakuwa Bize na kazi yake, lakini hapa mnaweza kubadilisha mawili matatu nakuweza kubadilisha mawazo, alisema
 
Sisi wana wa NMB tunaimani wafanyakazi wa Muhimbili wana watoto, kwahiyo tumewaletea bidhaa adimu ya mototo Akaunt ambayo unaweza kuifungua pale kwetu katika Tawi letu lililopo Muhimbili, alisema
 
Ninaimani pale kwetu tunavibanda kama sita ambavyo kuna wahudumu na ukifika pale utamwambia muhudum unahitaji huduma hiyo na atakuletea fom na utaijaza na kingine siolazima kwa wewe kuja Benk kuja kuweka pesa.
 
Utajazishwa fom ambayo ikifika tarehe ambayo uliambia benk utakumbushwa na ile pesa itatoka kwenye Akaun yako na itakwenda kwenye Akaut Mtoto. alisema Menena huyo.
 
Huduma hiyo nimbure kabisa kwani kwakufanya hivyo nikuwaandalia watoto wetu msingi bora wa maisha na kuwaandalia ufanisi wao katika masomo yao ya kila siku.
 
Karibuni sana na ninaomba tuendelee kushirikiana asanteni sana
 
  
Mkurugenzi wa Uuguzi, Agnes Mtawa akiwaonyesha zawadi aliyokabidhiwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Segla Mgaya (wa kwanza kulia) iliyo andaliwa wauguzi hao

Afisa Muuguzi, Agnes Kaberege akifungua  Shampeni

 
Mkurugenzi wa Uuguzi akiwasalimia wauguzi na kuanza kwa kumshukuru Mungu kwa kuwepo mahala hapa kwa siku ya leo,
 
Mtawa alisema, nijambo la kihistaria mimi tangu niingie kufanya kazi hii katika Hospitali ya Taifa Muhimbili sikumbuki kufanya kitu kama hiki,
 
Kwakweli nawashukuru kwa kubuni wazo kama hili na kwa sisi tuliyofika hapa na ninajuwa wauguzi tupo wengi lakini niwachache walioitikia wito na ninafikiri huu ni mwanzo mzuri,
 
Mungu akitupa Uzima wakati mwingine hapa patakuwa hapana nafasi ya kucheza pamoja na mvua nyingi lakini mmeweza kujitowa kwa kuja mahali hapa, alisema Mtawa
 
Nawaomba nduguzangu Wauguzi tuendelee kuwa na umoja kwa kushikamana kama tulivyoonyesha siku ya leo, tuendelee kupendana, kupeana nguvu kwa sababu kazi yetu kama mnavyo ijuwa kunachangamoto nyingi,
 
Lakini tukiwa kama mahala kama hapa tunacheza na kufurahi ausio jamani? kwa kuangalia Bahari na yale mabo mengine mengine tumeyaacha getini, kwahiyo pamoja na shukrani nyingi nawaomba tufurahi kwa pamona, alisema Mtawa kwa kumalizia ,
 
Leo si siku ya hutuba ni siku ya kufurahi 





Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi, Segla Mgaya (kulia)  akimkabidhi zawadi Mkurugenzi wa Uuguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili Agnes Mtawa, wanaoshuhudia ni wanakamati
Mkurugenzi wa Uuguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili, Agnes Mtawa (wa nne kulia) walio kaa katika picha ya pamoja na kamati ya maandalizi ya Sherehe hiyo
Mkurugenzi wa Uuguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili, Agnes Mtawa (wa nne kulia) walio kaa katika picha ya pamoja na kamati ya maandalizi ya Sherehe hiyo
Mkurugenzi wa Uuguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili, Agnes Mtawa (wa tatu kulia) walio kaa katika picha ya pamoja na viongozi wa Benk ya NMB






Sunday, April 16, 2017

MWENYEKITI U.W.T MGENI RASMI KATIKA MAHAFALI YA DINI YA KIISLAMU TAMBAZA DAR ES SALAAM JANA

 Mkuu wa Idara ya Biashara na Mlezi wa Wanafunzi wa Sekondari ya Tambaza, Abdul aziz Said  akizungumza na Wazazi  na wahitimu wa shule hiyo wakati wa Mahafali ya  Elimu ya Dini ya kiislam ya Sekondari ya kidato cha sita katika hafla iliyofanyika  Shule hapo Dar es Salaam jana. kulia ni Amiri wa Daawah Msikiti wa Tambaza, Sayed Qadry. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA) Mmiliki wa ujijirahaa blog.
 Mwanafunzi wa Kidato cha Sita, Maulidi Kassanga akisheherehesha kwa kusoma tenzi katika Mahafali hayo Dar es Salaam jana
 Wahitimu wakiwa katika utulivu wakisikiliza kwa umakini
 Wazazi na ndugu wakifatilia kilichokuwa kikiendelea ukumbini hapo
 Baadhi ya Wanafunzi hao
 Naib Imamu Msikiti wa Maamur, Haroub Khamis (kushoto) akizungumza jambo wakati wa hafla ya Mahafali ya Dini ya kiislam ya Sekondari ya kidato cha sita yaliyofanyika  Shule hapo Dar es Salaam jana ambapo wanafuzi hao wanajiandaa kufanya mitihani ya kumaliza kidato cha Sita
 Wanafunzi
 Mgeni rasmi katika mahafali hayo, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (U.W.T) Upanga Magharibi, Hajati. Joha Simba (mwenye mtandio mweusi kichwani) akifatilia kwa umakini na wakwanza kushoto ni Mwalimu wa shule hiyo, Zuhura Gajo
  Mwalimu , Zuhura Gajo akipokea risala kutoka kwa muhitimu, Juma Kassim baada ya kuisoma na kukabidhiwa mgeni rasmi katika mahafali hayo, ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (U.W.T) Upanga Magharibi, Hajati. Joha Simba (kulia)
 Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (U.W.T) Upanga Magharibi, Hajati. Joha Simba (kulia) akimkabidhi cheti mwanafunzi, Tausi Mohammed wakati wa hafla ya Mahafali ya Dini ya kiislam ya Sekondari ya kidato cha sita yaliyofanyika  Shule hapo Dar es Salaam jana ambapo wanafuzi hao wanajiandaa kufanya mitihani ya kumaliza kidato cha Sita
 Wanafunzi hao wakiomba Dua wakati walipokuwa wakimaliza mahafali hayo Dar es Salaam jana

 Amiri wa Daawah Msikiti wa Tambaza, Sayed Qadry (kulia) akizungumza na Wazazi na wanafunzi wakati wa Mahafali ya Dini ya Kiislamu katika Shule ya Sekondari ya Tambaza yaliyofanyika Dar es Salaam jana, kushoto ni  Mkuu wa Idara ya Biashara na Mlezi wa Wanafunzi wa Sekondari hiyo, Abdul aziz Said
Amiri wa Daawah Msikiti wa Tambaza, Sayed Qadry (kulia) akimkabidhi cheti, Rajab Kassim wakati wa hafla ya Mahafali ya Dini ya kiislam ya Sekondari ya kidato cha sita yaliyofanyika  Shuleni hapo Dar es Salaam jana ambapo wanafuzi hao wanajiandaa kufanya mitihani ya kumaliza kidato cha Sita
Rajab Kassim (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na marafiki zake mara baada ya kumalizika mahafali hayo Dar es Salaam jana
Rajab Kassim, (wa pili kushoto) wakiwa katika nyuso za furaha mara baada ya kumalizika mahafali hayo jana