Sunday, January 7, 2018

ALIYEKUWA KIONGOZI KITENGO CHA MAGONJWA YA DHARULA CHUMBA CHA UPASUAJI HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI (MNH), AWAPIGA MSASA WAFANYAKAZI WA KITENGO HICHO



Aliyekuwa Kiongozi wa Kitengo cha Magonjwa ya Dharula Chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Josephine Lwambuka amewaomba wafanyakazi hao hasa walio katika kitengo hicho kwa kujituma na kujitoa kwa kufanya kazi na kusimamia misingi ya sheria na kanuni kwa kufanya kazi kwa bidii.Lwambuka aliyasema hayo wakati alipokuwa akipongezwa kwa kuagwa na wafanyakazi wa kitengo hicho alichokuwa akikitumikia kama kiongozi alisema , Nduguzangu ninawaomba mshirikiane kwa umoja katika majukumu ya kazini na muwe wamoja na kupendana bila kubaguana na msiweke makundi yoyote, pia alisema, Lwambuka.
Naomba niwaambie kwa mtu yoyote hakuna anaye muona ila Mungu anamuona kwa kila hatua,
hivyo mfanyapo kazi msimsahau Mungu na kutosahau Ibada nawaomba hasa vijana kufanya kazi
kweli na akatoa tano akisema, Mimi mwenyewe toka nianze kufanya kazi na hadi Nastaafu
sijawahichukua kitu chochote kwa mgonjwa au kwa ndugu wa mgonjwa (Rushwa) na pia  nawaombeni  kusema ukweli daima kwani ukiwa muongo utakuja sahau  ulicho kisema hatimae
unaingia katika jambo ambalo lilikuwa lahitaji ukweli pasina kuficha, nawaomba muwe wakweli na uongo muutenge mbali katika kufanya kazi kwa kumsaidia Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali yetu ya Taifa,Nawaombeni mshirikiane kwa umoja na mumtangulize Mungu mbele mtafanikiwa bila kusahau kujishughulisha na kitu mbadala si kutegemea mwisho wa mwezi asanteni sana kwa kunifanyia shughuli namuomba Mungu awazidishie, pale mlipopunguza azidishe bila idadi nawapenda wote  asanteni. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)














 Mstaafu, Josephine Lwambuka akiwa katika picha ya pamoja katikati na aliye achiwa kijiti cha Kitengo cha magonjwa ya dharula chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili, Faustina Kissinde kushoto na Kiongozi Msaidizi wa  Kitengo hicho Mama Mchungaji, Flora Ndulango kulia
 Mstaafu, Josephine Lwambuka katikati akiwa katika picha ya pamoja na watoto wake na baadhi ya marafiki na wafanyakazi wa Hospitali ya taifa Muhimbili (MNH)
 Mstaafu, Josephine Lwambuka akiingia ukumbini

 Rafiki kipenzi wa Mama Lwambuka, Joyce Chirwa akipungia mikono waalikwa mara alipotambulisha

 Mstaafu, Josephine Lwambuka (wa pili kushoto) akijiburudisha na wafanyakazi wa Kitengo cha Magonjwa ya Dharula Chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), wakati alipokuwa akipongezwa katika ukumbi wa Salender Pub uliopo Upanga, Hafla iliyo andaliwa na Wafanyakazi wa Kitengo hicho
 Mstaafu, Josephine Lwambuka (wa pili kulia) akicheza na wafanyakazi hao
 Kiongozi Msaidizi Kitengo cha Magonjwa ya Dharula Chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Mama Mchungaji, Flora Ndulango (kulia) akifungua sherehe kwa Sala
 Muuguzi katika Kitengo cha Magonjwa ya Dharula Chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Charles Maungu akitambulisha baadhi ya wafanyakazi hao waliofika katika hafla hiyo
Mstaafu, Josephine Lwambuka (katikati) akipungia mikono wageni waalikwa mara baada ya kutambulishwa na Muuguzi katika Kitengo cha Magonjwa ya Dharula Chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Charles Maungu (pichani hayupo).
 Mkuu wa Kitengo cha magonjwa dharula chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili, Faustina Kissinde akipungia mikono wage waalikwa katika hafla fupi iliyoandaliwa na kitengo hicho ambapo katika kamati hiyo alikuwa Mwenyekiti
 Mkuu wa Kitengo cha magonjwa dharula chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili, Faustina Kissinde alianza kwa kumshukuru Mungu kufikia hapo walipofikia yeye na kamati yake yote na kusema namuomba Mungu azidishe umoja na upendo kati yetu na pili namshukuru muagwa mama, Lwambuka kwa malezi na ushauri wake na nitahakikisha hakuna hata mmoja nitakaye mpoteza kati ya watu ulio niachia kwani nitahakikisha anashirikiana nao kwa hali na mali, Kisinde alisema, Jambo la kujivunia kwa mama huyu ni kuiga yale yote mazuri aliyokuwa akiniambia kabla ya kustaafu kwake, kwanza kujitoa, kujitambua kama ni kiongozi niwazi kusikiliza ushauri na mawazo mazuri na kutatua changamoto na kuwasikiliza wafanyakazi wenzangu, Mama Lwambuka nitakuomba usisite mara nitapokuja kwako kuomba ushauri alisema kissinde.
 Mstaafu, Josephine Lwambuka (katikati), akigonganisha Glas na baadhi ya wafanakazi wa Kitengo  cha magonjwa ya dharula chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili wakati wa hafla fupi ya kumpongeza kwa kustaafu kwa mujibu wa sheria katika Ukumbi wa  Salender Pub uliopo Upanga

 Mmoja wa wafanyakazi katika kitengo hicho akicheza mziki wa kwao wa kiasili akirukaruka mfano wa chura


 Mstaafu, Josephine Lwambuka (katikati), akigonganisha Glas na baadhi ya wafanakazi wa Kitengo  cha magonjwa ya dharula chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili wakati wa hafla fupi ya kumpongeza kwa kustaafu kwa mujibu wa sheria katika Ukumbi wa  Salender Pub uliopo Upanga
 Mkuu wa Kitengo cha magonjwa dharula chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Faustina Kissinde (kulia) akishirikiana kukata Keki na aliye wahi kuwa Mkuu wa kitengo hicho, Josephine Lwambuka






Aliyekuwa Kiongozi wa Kitengo cha Magonjwa ya Dharula Chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Josephine Lwambuka akilishana kipande cha Keki na
Kiongozi Msaidizi Kitengo Mama Mchungaji, Flora Ndulango kwa mtindo wa kuukaribisha mwaka 2018





 Kiongozi Msaidizi Kitengo cha Magonjwa ya Dharula Chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Mama Mchungaji, Flora Ndulango (wapili kushoto) akiongozana na wafanya kazi wenzake kumpongeza aliyekuwa Mkuu wa Kitengo hicho, Josephine Lwambuka
 Baada ya kutunzwa Mstaafu, Josephine Lwambuka akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi hao

Mkuu wa Kitengo cha magonjwa dharula chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Faustina Kissinde akiongoza wafanyakazi wenzake kwenda kutoa zawadi ya kitengo chake iliyoandaliwa na kamati

 Mkuu wa Kitengo cha magonjwa dharula chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Faustina Kissinde akiongoza wafanyakazi wenzake kwenda kutoa zawadi ya kitengo chake iliyoandaliwa na kamati, Mstaafu akikabidhiwa bahasha kwa mstaafu,  Josephine Lwambuka (kushoto)



Aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha magonjwa dharula chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili, Josephine Lwambuka akibebwa juu kwa ishara ya kuonyesha kumkubali katika utendaji wake wa kazi


Rafiki Kipenzi wa Mstaafu Mama Lwambuka akizungumza jambo katika hafla hiyo
Mkuu wa Kitengo cha magonjwa dharula chumba cha Upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Faustina Kissinde akiwashukuru wote walio husika na kufanikisha Sherehe hiyo





No comments:

Post a Comment